Na Ulanga Ally
Natanguliza pole kwa familia na wanamageuzi kwa msiba wa mpiganaji mwenzetu Bi. Regia Mtema. Hakika msiba huu nipigo kubwa kwa Taifa. Tunamuomba Mwenyezi Mungu amuweke mahali pema peponi,amina.
Dr. Slaa ukiwa kiongozi mwenye sura ya kitaifa, utambue kuwa maisha yako yote yanakuwa mikononi mwa jamii (watanzania).Hii na maana ya kwamba kwa lolote utakalo shughulika nalo lazima litaifikia jamii na kupata fursa ya kulitafakari. Tunatambua kuwa kila mtu anatabia zake binafsi aidha kutokana na malezi, mafundisho ama kuzaliwa. Ni dhahiri pamoja na yote kuna tabia zisizokubalika (mbaya) na zinazokubalika (nzuri) katika jamii.
Tunatambua uligombea nafasi kubwa ya uongozi wa juu wa Taifa letu (U- Rais) na kwa bahati nzuri ama mbaya ulishindwa na Rais akapatikana naye ni Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete.
Tutambue kuwa kulingana na sheria zetu pamoja na Katiba tuliyo nayo huyu ndiye kiongozi wetu Watanzania na ndio maana kila mtu akimtaja anaanza na "Rais". Katika ushindani kuna kushinda na kushindwa na inapokuwa shida kupinga ushindi wa mtu ki-ushahidi na kimazingira ni busara kukubali kushindwa.
Hivi vitu kwako vimekuwa ni vigumu kuvikubali na katika hali ya kawaida umeonekana ni mtu mwenye chuki kubwa tena ya wazi kwa Rais wa nchi. Binafsi mwenendo wa tabia yako siupendi kwani umejaaa unafiki,wivu,chuki na majungu ambapo haipaswi kwa kiongozi wa Kitaifa kama wewe na zaidi mtu wa imani (Padri Mstaafu) kuwa nayo.
Tunatambua kuwa Kikwete kama Rais na kama binafsi ana mapungufu yake lakini hawezi kuwa mbaya kwa yote. Sidhani kwamba imefikia hatua tunajali ya KIJINGA na kuacha MEMA.Kitendo chako cha kumuona Rais wa Nchi kama adui yako namba moja kiasi cha kutosalimiana (nitafafanua chini) hata katika shughuli za kijamii ni aibu kwa taifa, kwako binafsi, kwa kiongozi wako Mbowe na Chama kwa ujumla. Sikuwa na waza juu ya muendelezo wa tabia yako lakini sasa nimebaini kuwa wewe si muungwana na haufai kuwa kiongozi wa Taifa hili kama hutobadilika. Mifano:-
1) Ulipinga matokeo ya uchaguzi kupitia vyombo vya habari kwamba si halali na hii ni kwa sababu hukushinda. (Watanzania tulikusikia na kukuona).
2) Ulikataa kuhudhuria katika mwaliko wa kumtangaza Kiongozi aliyeshinda U-Rais huku na wewe ukiwa mgombea. (Watanzania tulikusikia).
3) Mchakato wa Katiba hukushiriki kwenda kumuona Rais Ikulu huku ukiwa kiongozi na mratibu Mkuu wa Chama kwa nafasi yako ya Ukatibu Mkuu. (Watanzania tunajua).
4) Umekataa kuhudhuria Sherehe zote za Kitaifa hasa pindi chama kinapoalikwa na kukuteua wewe kuhudhuria.
5) Kumkwepa Rais wa Nchi katika Msiba wa kipenzi chetu Bi. Regia Mtema (Hili limenisikitisha kuliko yote) huku ukiwa na taarifa ya ujio wake na baadae kuwasili baada ya kusikia Rais ameondoka. (tunajua waweza sema kuwa ulikuwa na majukumu mengine).
Hizi tabia zako hazipaswi kuvumilika hata kidogo na ni zaidi ya unyama. Wewe kama Kiongozi unayejiamini ni kwa nini ujifiche ama umkimbie mtu unayemuona kama adui yako? (unapaswa ukabiliane nae) tabia hii inaonyesha mengi huwa unaidanganya jamii juu yake sasa ni AIBU kuonana nae uso kwa uso. Tambua maisha yako na ya viongozi wengine wa vyama vya kisiasa ndani ya Nchi hii yako mikononi mwa Watanzania na si kwao binafsi. Hivi kama ni kuku -assassinate unafikiri TISS wanashindwa? Ukweli ni kwamba wanaweza lakini watawaambia nini Watanzania juu ya kifo chako. Hii nimeisema kama unahisi kuonana na Kikwete ata katika MSIBA maisha yako yatakuwa hatarini.
Tunajua by implication wewe ni mfuasi wa vegeance policy hasa utakapo pata madaraka (U-rais) , lakini sidhani kusalimia na mtu kutakupunguza hasira na malengo yako ya kutochukua maamuzi unayoyapenda.
Regia Mtema (Marehemu) -Ametukutanisha hapa msibani kwa sababu ya uungwana wake kwa watu wote pasipo kujali itikadi ya vyama ama dini. Huyu alikuwa binti mdogo sana lakini kwa miaka 32 (umri wake) ameweza kufanya makubwa na kusababisha sote kumpenda. Regia angekuwa mbaguzi, mwenye chuki, asiyekubali kubadilika leo hii pamoja na msiba wake , lakini maneno mengi ya chini chini yangekuwa yakipita juu ya ubaya wake.
Dr. Slaa tunakuthamini kwa mchango wako wa mageuzi ya kisiasa, changamoto pamoja na umri wako (miaka 64 tarehe 29/10/2012 utatimiza). Hivi kweli kujitenga kwako ama kwa tabia hizi unatufundisha nini sisi vijana tunaokuwa na tegemeo la Taifa?
Nampongeza sana Mwenyekiti wa Chama Mhe. Freeman Aikaeli Mbowe hakika ni tofauti kabisa na wewe. Yote ambayo umekwepa kuyatekeleza ata amabayo yamekuwa yakikuhusu , yeye ameweza kuyatekeleza napengine si kwa nafasi yake bali kwa kujali utu na kutambua kuwa SIASA SI VITA (pale demokrasia inapochukua mkondo wake). Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kimepata kiongozi bora na mtu wa watu. Mhe. Freeman Mbowe hakika:-
1) Ni mpenda watu
2) Hana Makuu, majungu wala fitina
3) Ni binadamu wa kweli anayeishi kulingana na mwenendo wa maisha ulivyo.
4) Kiongozi bora wa Kisiasa na Kijamii
5) Hana visasi na mwenye kutambua utu wa mtu
6) Muungwana na si mgumu wa kusamehe
7) Mwenye msimamo thabiti wenye kujali haki za wananchi na Wajibu wa Watawala
8) Mtu wa kujichanganya na wengine pasipo kujali cheo chake, madaraka yake na pesa zake. “Ewe Mwenyezi Mungu tunakuomba umzidishie Umri pamoja na Busara Kiongozi huyu.”
WITO
Dr. Slaa tunajua ni jinsi gani ilivyo ngumu kubadili tabia yako hasa katika utu uzima ulio nao,lakini hakuna kinachoshindikana mbele ya Mungu. Rudi nyuma utubu na Mwenyezi Mungu atakupa busara ya kutuongoza vinginevyo "Your leadership can be another disaster to our Nation".