NG'WANAKANUNDO - MANJU MASHUHURI WA KISUKUMA KUTOKA MWANZA

Wednesday, April 29, 2009

MWALIMU NYERERE - NABII ALIYEHUBIRI NA KUTENDA ALICHOKIHUBIRI

Makala hii imetoka katika gazeti la Jamii Kwanza la Jumanne (28/4/2009).
===========================================
Mwalimu Nyerere: Nabii Aliyehubiri na Kutenda Alichokihubiri
 Dkt. Masangu Matondo Nzuzullima
 
Mengi yameshasemwa kuhusu Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika siku za hivi karibuni hasa kutokana na tamasha lililoandaliwa na wanazuoni wa Tanzania wakishirikiana na wenzao wa nje. Lengo langu katika makala hii siyo kurudia ambayo tayari yamekwishasemwa juu ya Mtanzania huyu hodari bali ni kumtazama Mwalimu Nyerere kutokana na maneno yake mwenyewe na kauli zake mbalimbali. Nimeamua kufanya hivyo baada ya kukipata na kukisoma kitabu chake cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania ambacho alikiandika mwaka 1993 na kuchapishwa na Zimbabwe Publishing House. Hiki kilikuwa ni kipindi ambacho nchi ilikuwa inapita katika misukosuko ya kiuongozi na Muungano wa Tanzania na Zanzibar ulionekana kuwa hatarini kutokana na kuibuka kwa kundi la wabunge waliokuwa wakidai serikali ya Tanganyika.

Mwalimu Nyerere alisimama kidete kuupigania Muungano na kuhakikisha kwamba nchi yetu inapita katika msukosuko huu kwa usalama. Akiamini kwamba "Tanzania ni lulu ya pekee kabisa katika historia ya Afrika huru" kwani "Nchi nyingine zote ni za kurithi kutoka katika Ukoloni" wakati "Tanzania ni ya kuundwa na sisi wenyewe, kwa hiari yetu wenyewe, baada ya kukomboa sehemu zake mbili kutoka ukoloni" (Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania, uk. 57), Mwalimu hakuwa tayari kukaa pembeni na kushuhudia nchi ikiserereka kuelekea gema la hilaki . Hapa chini ni kauli zake mbalimbali kuhusu mambo mbalimbali ya muhimu yaliyokuwa yakilikumba taifa katika kipindi hiki. Katika kauli hizi unaweza kuuona uwezo wake wa kinabii, uwezo wa kuona mbali na kupima mustakabali wa nchi kwa darubini kali ya fikra na hali halisi ya wakati uliopo; ukweli usio na hofu pamoja na upendo wa kweli kabisa aliokuwa nao kwa Tanzania yake aliyoipenda. Kauli zote hizi zinatoka katika kitabu nilichokwishakirejerea hapo juu: Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania, Zimbabwe Publishing House, 1993.
Aliposikia tetesi kwamba baadhi ya wakereketwa wa CCM walikuwa wameanza kampeni za kutaka rais Mwinyi aongezewe vipindi vya muda wa kuwa rais, Mwalimu Nyerere hakupendezwa na jambo hilo na mara moja alikwenda kwa Rais Mwinyi na kumsihi azizime kampeni hizo. Pia aliwatafuta viongozi wa kampeni hizo na kuwaomba wasilifuatilie jambo hilo. Aliposikia kwamba jambo hilo la rais Mwinyi kuongezewa vipindi vya kuwa rais lilikuwa bado linazungumzwa hata baada ya juhudi zake kulizima alikereka na kusema maneno yafuatayo:

"Plato, Myunani wa kale, alipendekeza kuwa mafilosofa ndio wanaofaa kuwa watawala wa nchi, maana wana sifa mbili muhimu: kwanza wana uwezo wa kutawala, na pili hawapendi kutawala. Kwa hiyo Jamhuri ya Plato itakuwa na sheria ya kuwalazimisha mafilosofa kutawala kwa zamu; na mtu zamu yake ya kutawala ikiisha, atafurahi sana kurudia shughuli zake za falsafa ambazo ndizo hasa anazozipenda. Lakini nchi zetu hazitawaliwi na mafilosofa wa Plato; watawala wetu ni wanasiasa wa kawaida ambao wanapenda sana kutawala, hata kama hawana uwezo wa kutawala; na ambao wako tayari hata kuhonga ili wachaguliwe kuwa watawala, na wakisha kuchaguliwa hawatoki bila kulazimishwa. Si busara kuwaachia wao wenyewe ndio wawe waamuzi wa lini waache kuwa watawala" (ukurasa wa 8)

Utabiri huu unaendelea kutimia. Chaguzi zetu sasa (hata zile za udiwani tu) zimegeuka kuwa miradi ya watu matajiri tena inayoghalimu mabilioni ya shilingi. Kule Bariadi Magharibi katika uchaguzi uliopita mgombea mmoja alikuwa anagawa pesa, chumvi, sukari, kanga,vitenge, mabati, baisikeli na hata pikipiki. Kwa vile, kama wasemavyo wazungu, "there is no free lunch:" "hakuna cha bure", mabilioni haya ni mradi wa mtu na ni lazima yarudishwe siku moja. Halafu wanasiasa hawa wakija kuibuka na "vijisenti" vyao, tunapiga makelele na kushangaa utadhani kwamba hatukujua. Rushwa katika chaguzi zetu ni tatizo kubwa linalofuta kabisa maana nzima ya demokrasia na kuzigeuza chaguzi hizi kuwa bidhaa tu zinazoweza kununuliwa na watu wenye mapesa yao.
 
Katika hoja ya kugombea serikali ya Tanganyika, hoja ambayo Mwalimu aliipinga kwa nguvu zake zote, aliyevishwa lawama ni waziri mkuu (pamoja na katibu mkuu wa CCM) wa wakati ule. Lakini pia alikerwa zaidi na kushindwa kwa raisi Mwinyi kumfukuza kazi waziri wake mkuu kutokana na kigeugeu alichokionyesha kwa kupinga hoja ya serikali ya Tanganyika bungeni na baadaye kubadili msimamo na kuunga mkono hoja hiyo. Alisema yafuatayo kuhusu jambo hili:

"Waziri Mkuu si mpishi wa Rais, hata tuseme kuwa maadamu Rais mwenyewe anayapenda mapishi yake, sisi wengine tusipoyapenda si kitu. Waziri Mkuu ni Mpishi Mkuu wa Tanzania nzima. Kama hatupendi mapishi yake, au kaanza kutupakulia vyenye sumu, au kachoka, au kashindwa kupika, ni wajibu wetu kumwambia Mwajiri wake ateue mpishi mwingine."(ukurasa wa 48).

Kwingineko anaendelea kusema hivi kuhusu jambo hili.

"Pengine inafaa niseme kwamba inashangaza na kutisha kidogo kuona kuwa kujiuzulu kwa Waziri ye yote kunafanywa kuwa ni jambo la kuvutana au la kubembelezana...lakini hata hivyo ni jambo la kushangaza kidogo kwamba Viongozi wetu wa Mageuzi, hata bado hatujafa, wanaona kuwa ni kosa kuwakumbusha kuwa vyeo walivyo navyo ni dhamana. Wanadhani kuwa uwaziri ni usultani: ukisha kuwa sultani utakufa sultani! Nadhani wanakosea. Nchi hii imewahi kung'oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wa kuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa" (ukurasa wa 45)
Sote tunajua kwamba ukishakuwa waziri basi ni nadra sana kufukuzwa kazi. Hata uboronge vipi, hasa hasa utaambulia kubadilishwa wizara tu na au kupangiwa kazi nyingine. Hata hivyo jambo hili limeanza kuchukua sura mpya kutokana na kushuhudia kwetu mawaziri kadhaa wakiwajibika na kujiuzulu wenyewe. Hili, kwa maoni yangu, ni jambo jema linaloonyesha kwamba, japo safari yetu bado ni ndefu, demokrasia yetu changa inazidi kuimarika.
Mwalimu Nyerere pia hakuogopa kusema ukweli, hata kama ulikuwa ukweli mkali tatanishi. Hakukubali kukaa kimya huku akishuhudia nchi ikiyumbayumba. Kuhuhu uwezo wa Rais Mwinyi kutawala na utaratibu mzima wa marais kukabidhiana madaraka kwa usalama alisema yafuatayo:

"Rais Mwinyi ni mtu mwema na mpole, lakini ni kiongozi dhaifu; na upole wake na udhaifu wake unatumiwa na watu ambao wala si wema wala wapole kuhatarisha umoja na amani ya nchi yetu. Kipindi chake cha pili kinakaribia kwisha...Kwa sababu ya minong'ono-nong'ono ya watu wasioona mbali kuhusu Rais, na kubabaishwa anakobabaishwa na washauri wake wakuu, nililazimika kuiambia wazi wazi Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi kwamba najiona kuwa ninao wajibu wa kumsaidia Rais amalize kipindi chake salama. Kipindi cha mpito, cha kujaribu kujenga utaratibu wa kikatiba wa kubadili uongozi wa nchi yetu kwa heshima na amani hakitakamilika mpaka hapo Rais Mwinyi atakapomaliza kipindi chake kilichobaki kwa usalama, na kumkabidhi madaraka Rais mpya kwa utaratibu ule ule uliompa madaraka hayo" (uk. 50-51)

Katika kipindi hiki serikali ilionekana kuwa imeparaganyika na kukosa mwelekeo na Mwalimu Nyerere aliamini kuwa ubovu wa uongozi katika Chama cha Mapinduzi na serikali yake ulikuwa umefikia kileleni kabisa. Unaweza kuiona hasira yake katika maneno yake yafuatayo:

"Waingereza wana msemo: "Nature abhors a vacuum", "hulka huchukia ombwe". Hata siasa huchukia ombwe. Kama uongozi ni mbovu, upo kama haupo, au upo kwa maslahi ya wenyewe, watatokea watu waujaze uwazi uliopo; hauwezi kuachwa wazi hivi hivi. Lakini uongozi mbovu ni kama mzoga, una tabia ya kukaribisha mafisi na mainzi. Tusidhani kuwa hulka ya siasa yetu ni tofauti na hulka ya siasa ya watu wengine; kwamba sisi tunaweza kuvumilia uongozi mbovu na tusivune matunda ya hulka ya uongozi mbovu" (uk.52)

Katika suala hili anaendelea kusema yafuatayo:

"Kwa maana moja sasa hatuna serikali, tuna mawaziri tu. Serikali ni timu; na timu halisi ina dira na rubani. Mkusanyiko wa mawaziri bila mwelekeo, bila mwongozo, bila mshikamano na bila uongozi, kila Waziri na lwake, hauwezi ukaitwa serikali. Katika hali kama hiyo, hata bila ubovu mwingine wa nyongeza mambo muhimu ya Nchi hayawezi kujadiliwa wala kushughulikiwa" (uk.53)

Kwingineko aliwaonya wananchi kutowaogopa viongozi wao kwani viongozi wanapaswa kuheshimiwa na siyo kuogopwa. Na wanapotenda mambo ya haramu kama hili la kutaka kuunda serikali ya Tanganyika basi wananchi inabidi wakatae kwani kufanya hivyo ni haki yao.

"Kukubali kufanywa vikaragosi vya Viongozi ni dalili ya woga, si dalili ya heshima; na woga na heshima ni vitu viwili mbali mbali. Maadili mema yanatutaka tuwaheshimu Viongozi wetu, madhali wanajitahidi kutimiza wajibu wao. Maadili mema hayatudai tuwaogope Viongozi wetu. Na viongozi makini hupenda kupata heshima ya wananchi wenzao, lakini hawapendi kuogopwa. Kuogopwa ni sifa na ada ya madikteta, viongozi halisi hawapendi kuishiriki. Kujenga mazoea ya kutii viongozi hata katika mambo haramu ni dalili ya woga, ni kukaribisha udikteta." (uk.65)

Mwalimu Nyerere alikuwa amechoshwa na ubovu wa uongozi katika Chama cha Mapinduzi na hata mustakabali wa kisiasa na kiuongozi ndani ya vyama vya upinzani. Tazama kauli zake hizi zinavyobakia kuwa sahihi hata leo – miaka zaidi ya 15 tangu azitoe!

"Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi haiwezi kuepuka lawama. Lakini kuilaumu Kamati Kuu ni kukiri kwamba sasa Chama cha Mapinduzi kina kansa ya uongozi ambayo isipotibiwa itakiua Chama kizima. Pengine kwa Nchi yetu hili lisingekuwa jambo la kutisha kama tungekuwa tumeanza kuona Chama kizuri cha Upinzani ambacho kinaweza kuiongoza Nchi hii badala ya CCM. Hakijaonekana bado. Chama cha Mapinduzi, kwa sababu ya uzito wa historia yake, hadhi ya jina lake, mfumo wa wavu wake, mazoea ya watu, na ubovu wa Vyama vya Upinzani, kinaweza kuendelea kuchaguliwa na Watanzania, pamoja na kansa ya uongozi wake. Au watu wanaweza wakachoka, wakasema, "potelea mbali:" wakachagua Chama cho chote, ili mradi tu watokane na kansa ya uongozi wa CCM. Hainifurahishi kuyasema haya, lakini uhai wa Nchi yetu unataka yasemwe" (uk.61)

Akisisitiza jambo hili hili la kansa ya uongozi ndani ya CCM na ubovu wa Vyama vya Upinzani, Mwalimu Nyerere anasema yafuatayo:

"Nilisema awali kwamba kansa ya uongozi ndani ya Chama cha Mapinduzi isingekuwa ni jambo la kutisha sana kama tungekuwa tumeanza kuona Chama kizuri cha upinzani kinachoweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM. Ubovu wa uongozi ndani ya CCM ndio uliofanya nikapendekeza tuanzishe mfumo wa Vyama Vingi. Nilitumaini kwamba tunaweza kupata Chama kingine kizuri ambacho kingeweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM; au ambacho kingekilazimisha chama cha Mapinduzi kusafisha uongozi wake, kwa kuhofia kuwa bila kufanya hivyo kitashindwa katika uchaguzi ujao. Lakini bado sijakiona Chama makini cha upinzani; na wala dalili zo zote za kuondoa kansa ya uongozi ndani ya CCM. Bila upinzani mzuri wa nje, na bila demokrasia halisi ndani ya Chama cha Mapinduzi, Chama hiki kitazidi kudidimia chini ya uzito wa uongozi mbovu. Kwa hali yetu ya kisiasa ilivyo nchini hili si jambo la kutarajia bila ya hofu na wasiwasi!" (uk.66)

Je, ni kipi ambacho kimeshabadilika hapa? Ati kansa ya uongozi ndani ya CCM ilishapatiwa tiba? Na vyama vya upinzani vimeshaboreka? Siwezi kuwasemea wanaCCM kwani wenyewe ndiyo wanajua kama wameshaitibu kansa ya uongozi ndani ya chama chao. Hata hivyo si lazima mtu uwe daktari kuweza kuona dalili wazi za mgonjwa anayetafunwa na kansa na dalili hizi bado zinaonekana ndani ya CCM. Misukosuko ya kashfa mbalimbali za ufisadi ni ushahidi tosha kwamba chama hiki kikongwe na chenye historia ya pekee katika nchi yetu bado kinaugua na mambo si salama ndanimwe kiasi kwamba kwa mara ya kwanza inasemekana kwamba makundi kinzani yamezuka mumo kwa mumo – makundi ambayo yanatishia kukidhoofisha. Kuhusu hali ya wapinzani hili si jambo la mjadala: Mwalimu Nyerere alikuwa sahihi. Kwa maoni yangu, bado hakuna Chama kizuri cha Upinzani ambacho kinaweza kuiongoza nchi badala ya CCM; na kwa vile wapinzani hawa wameshashindwa kabisa kuungana na kusimamisha mgombea mmoja, sidhani kama wanayo nafasi kubwa ya kushinda na kuongoza nchi katika uchaguzi wa mwakani. Lakini, jambo jingine linaweza kutokea: wananchi wanaweza kusema, "potelea mbali, liwalo na liwe" na wakachagua Chama cha Upinzani.

Sijui kama kitabu hiki cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania kinapatikana madukani. Ni kitabu kizuri ambacho kinafaa kisomwe na kila Mtanzania mpenda demokrasia, uhuru wa mawazo na anayeipenda na kuitakia mema nchi yake.

Napenda nimalizie kwa kusema kwamba Mwalimu Nyerere alikuwa binadamu kama sisi na alitenda makosa. Kwa mfano sote tunajua kwamba siasa zake za Ujamaa na Kujitegemea zilishindwa. Lakini hata alipotenda makosa, nia yake ilikuwa njema na alitanguliza maslahi ya nchi. Mwalimu Nyerere aliamini na kutenda alichokihubiri. Ndiyo maana hakujilimbikizia mali na kujitajirisha yeye pamoja na familia yake kama tunavyoshuhudia leo kwa baadhi ya wanasiasa wetu walafi. Na huyu ndiye Mwalimu Nyerere ninayemfahamu mimi – mwanasiasa mwadilifu, msomi na mwanafalsafa makini aliyeipenda na kuipigania nchi yake, bara zima la Afrika na wanyonge popote walipo ulimwenguni. Nyerere aliyehakikisha kwamba hata sisi watoto wa wakulima kutoka vijijini tunapata elimu kwani aliamini kwa usahihi kwamba elimu ndiyo mkakati-mama katika ukombozi wa jamii yo yote ile. Nyerere aliyetuwekea misingi thabiti ya umoja, undugu na Utanzania – misingi ambayo imetuwezesha kuishi kwa amani kwa miongo kadhaa tangu tupate uhuru. Nyerere msema kweli na ambaye alijaribu sana kuionya, kuipigania na wakati mwingine kuionyesha njia kinabii nchi yake kila mara ilipoonekana kuwa katika hatihati. Huyu ndiye Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wangu – Mtanzania halisi na Nabii aliyehubiri na kutenda alichokihubiri!

Monday, April 27, 2009

UBAGUZI WA RANGI TANZANIA (INASIKITISHA SANA)

Hapa sina la kusema lakini kama ulishawahi kwenda kwenye hizi hoteli zinazoitwa za kitalii na ngozi yako nyeusi basi bila shaka utakuwa umeshakumbana na haya mambo ya ubaguzi - kwa viwango tofauti tofauti. Nilikwenda pale Kempsink na nilichunguzwa kuanzia nilichovaa na jamaa waliudhika niliposema kwamba sifahamu Kiingereza. Walitulia tu kidogo pale nilipowaambia kwamba nilikuwa nalipa dola keshi. Kwa nini tubaguliwe katika nchi yetu wenyewe?

============================================================

Racism within TZ as Arusha hotel denies access to Blacks

2009-04-26 13:18:37

By Adam Ihucha, Lake Manyara

Manyara-born conservationist David Maige, plus members of his family, had a nasty experience recently, which will be etched on their memories for probably the rest of their lives.

The man, a Tanzanian national employed by Lake Manyara National Park, took his family to the legendary Lake Manyara Hotel for a leisurely outing that turned out to be an nightmarish anti-climax.

Upon approaching the main gate of the prestigious lodge, watchmen relayed a piece of information to him which didn`t register immediately as being factual - that the facility was a no-go zone for natives, but the preserve of foreigners and members of the power elite.

Lake Manyara Hotel is one of the formerly government-owned prestigious lodges in the northern tourist circuit, which was privatized a couple of years back and is now owned by Hotels & Lodges.

The hotel is located nearly 6 km west-south of Manyara National Park.


On Thursday this last week, the conservationist disclosed the experience to Natural Resources and Tourism Minister, Shamsa Mwangunga.

``Honourable Minister, as domestic tourists, Tanzanians are facing discrimination at the hotel.

We are not allowed to approach the facility, let alone getting in and being served,`` he lamented.

An irritated Minister Mwangunga paid a surprise visit to the hotel immediately, to establish the authenticity or otherwise, of the allegations.

Two of its senior officials -- Group Operations Manager Fred Tenga and General Manager Hamis Juma, put up spirited defence, saying that restrictions on access to the hotel were driven by security concerns, in the wake of terrorist attack threats.

``Our hotel is close to a residential area, and so we felt it necessary to control unnecessary influx, taking into account that we have suffered three robbery incidents, `` Tenga told the minister, stressing that security of their clients is one of the top in their agenda.

On his part, Juma told her that the restriction policy was imposed by the hotel management following attacks on some hotels in the East African region and elsewhere in the world.

``Since terrorists have no labels, the management decided to restrict an influx of local people into the lodge,`` the hotel boss noted.

Responding, the shocked minister said the move was not only frustrating her ministry`s efforts to promote domestic tourism, but also contravened the laws of the land.

``Your theory is baseless; after all, these are Tanzanian facilities. How dare you bar them from having a nice time in their own hotel?`` Mwangunga asked.

The minister then issued a one week ultimatum for the management to revoke the policy and to give her a feedback.

A panicky Tenga apologized and said the policy was being withdrawn with immediate effect.

Constructed about 38 years ago, Lake Manyara Hotel, Seronera, Ngorongoro and Lobo lodges formerly belonged to the Tanzania Tourist Corporation (TTC) and were later handed over to Tanzania Hotels Investment when TTC was disbanded in 1992.

Some years back hotel and lodges were acquired by a local private firm, Hotels and Lodges Limited.

The firm spent between $14 million and $20 million to rehabilitate Lake Manyara hotel and Seronera, Ngorongoro and Lobo lodges.
  • SOURCE: Sunday Observer

Friday, April 24, 2009

WIMBO WA KISUKUMA - NAKUMBUKA NYUMBANI MIMI

....Shiliwa shiswe shazugagwa siza, shokejagi msiginogelwa...
...chakula chetu kimepikwa vizuri, msichoke kurudia tena...

video

KAMA BIBLIA INGEANDIKWA NA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU

Sasa ni mwisho wa muhula na tumemaliza madarasa jana. Hiki ni kipindi cha wanafunzi kuhaha, kuchanganyikiwa na kusononeka. Habari hii imetoka katika gazeti la wanafunzi na inajaribu kuonyesha (kiucheshi) jinsi ambavyo Biblia ingekuwa kama ingeandikwa na wanafunzi wa vyuo vikuu. Inaburudisha!
  • The loaves and fish would be replaced by 2-for-1 deals and stale chips
  • The 10 commandments would only be five, but they would be double-spaced and written in a large font so they'd look like 10.
  • The forbidden fruit would be eaten in one bite by a drunken frat boy on a dare
  • Wine would be replaced by beer for all sacramental purposes
  • Reason Cain killed Abel: they were roommates.
  • Final exams would be the first sign of the apocalypse
  • The Tower of Babel would be blamed for your foreign language credit requirement.
  • Instead of God creating the world in six days and resting on the seventh, he would put it off until right before it was due, then pull an all-nighter and hope no one noticed.

Thursday, April 23, 2009

KILA MTOTO AAMBIWE ANAWEZA - THE OBAMA STORY (NA DJ. GADHAFI)

Hii ni kuunga mkono mada ya Bwana Kaluse (bofya hapa) kwamba kufanikiwa na kutofanikiwa ni uchaguzi wetu wenyewe. The Obama Story ni uthibitisho tosha wa dhana hii. Kila mtoto na aambiwe kwamba anaweza na awezeshwe kufikia ndoto yake. Tutaona maajabu katika jamii!

video

Wednesday, April 22, 2009

BONDIA MSHINDI NA MUNGU WAKE

Huyu bondia aliyeshinda naona anaomba na kumshukuru Mungu wake kwa kumwezesha kumfletisha bondia mwenzake. Huyo aliyefletishwa naye akipata fahamu sijui atamlaumu Mungu kwa kuruhusu afletishwe na mpinzani wake au pengine atachukua mtazamo chanya na kumshukuru Mungu kwa kufletishwa kwake akijipa matumaini kwamba kufletishwa huko kutakuwa funzo kubwa katika mapigano yake yajayo. Imenifurahisha kuona jinsi Mungu anavyogawa "mibaraka" yake kama bondia huyu anavyotudhihirishia; na sisi binadamu tunavyoipokea mibaraka hiyo!

Tuesday, April 21, 2009

WANAMAGEUZI WANAOGEUKA

Wakati akianzisha sera zake za Utanganyika na magabacholi, mwanasiasa huyu alikuwa machachari na maarufu sana. Alikuja pale Chuo Kikuu Mlimani na alibebwa juu juu kutoka ukumbi wa Nkrumah. Leo hii hakuna mtu anayemchukulia kuwa siriazi na amegeuka kuwa "mropokaji" tu. Hata moto wa Lyatonga ambao ulikaribia kuwaunguza CCM sasa umeshazimika. Je, Wanamageuzi hawa wanaogeuka, wana nafasi yo yote ya kuchukua madaraka mwaka kesho?

Monday, April 20, 2009

VIJANA WETU "WATUNDU" TUNAWASAIDIAJE?

Ni kweli kwamba elimu yetu haitupi utundu na maarifa ya kuweza kujiajili. Tunategemea kuajiriwa baada ya kuhitimu. Ni kweli pia kwamba elimu yetu ni butu na haizichokonoi akili zetu na kuchochea udadisi wetu mpaka tukafikia kilele cha umakinifu na welewa wetu . Tunakariri tu, tunashinda mitihani, tunahitimu na kwenda kuukabili ulimwengu hivyo hivyo...Mbali na matatizo yote haya, bado tuna vijana wenye vipaji ambao, hata bila elimu hii tuijuayo, wameweza kufanya ugunduzi na kujitengenezea vifaa ambavyo vimethibitishwa kisayansi kuwa vinafanya kazi. Mfano ni huyu kijana hapo kwenye picha. Je, wagunduzi wetu hawa wanapata msaada wo wote wa kitalaamu (au kifedha) kuweza kuwaendeleza? Au ni yale yale ya kuoneana wivu, kupigana vita na kutokomezana? Kijana huyu anaingiza karibu sh. 45,000 kwa siku kwa kuuza hizi antena ambazo mwenyewe anazitengeneza. Vipi kama angepewa kibanda, akasaidiwa kifedha na utaalamu zaidi? Sera yetu inasemaje kuhusu Watanzania wagunduzi kama huyu kijana? (Picha kutoka gazeti la This Day tarehe 18/4/2009 - ukurasa wa mbele - kupitia blogu nzuri ya Kennedy)

Thursday, April 16, 2009

KUSTAWI NA KUANGAMIA KWA JAMII

Umeshawahi kujiuliza ni kwa nini jamii zingine hustawi na zingine huangamia? Ni kwa nini kwa mfano dola kubwa kama Mayan liliweza kuangamia na kupotea kabisa? Alhamisi iliyopita (tarehe 9 April, 2009) nilihudhuria mhadhara ambao ulitolewa na Jared Diamond - mwandishi wa vitabu viwili mashuhuri kuhusu masuala ya kustawi na kuangamia kwa jamii (Collapse na Guns, Germs and Steel).

Mwandishi huyo anatumia vigezo vinne kuweza kubashiri ni jamii au dola gani ambazo zinayo nafasi ya kustawi na zipi zinaweza kuangamia (kama Historia inavyotufundisha). Vigezo hivi ni: hali ya mazingira, serikali, matumizi ya maliasili, marafiki na maadui. Alisema kwamba jamii ya binadamu na dunia nzima kwa jumla ni kama yai linaloengwaengwa huku na huko kwani katika jina la sayansi binadamu ameweza kujitengenezea na kujirundikia silaha ambazo zinaweza kumtokomeza asionekane kabisa katika uso wa dunia. Kama ataibuka kiongozi mwingine "mwehu" kama Adolf Hitler na kuamuru kutumia silaha za kinuklia basi jamii karibu zote hapa duniani zitaangamia. Hata hivyo alitupoza wasikilizaji wake kwa kutuambia kwamba kulingana na protokali zinazolinda silaha hizi, maangamizi yetu kutokana nazo pengine si jambo rahisi sana kutokea.

Kilichonivutia katika mhadhara huu - na ambacho hakitiliwi maanani sana katika vitabu vya Kihistoria, ni ukinzani wa kimatabaka ambao alisema ndiyo umeangamiza jamii na madola mengi pengine kuliko sababu nyingine yo yote. Alisema kwamba unapokuwa na jamii yenye watu wachache ambao ni matajiri kupindukia na umma ulio mwingi ukawa katika umasikini mkali, basi hizi ni dalili za mwanzo wa mwanzo wa kuangamia kwa jamii. Hawa masikini watavumilia lakini mwishowe uvumilivu wao utafika kikomo na hapo ama watagoma kuzalisha mali (ambayo ndiyo tegemeo kuu la dola) ama wataamua kupambana. Alisema na hapa nanukuu "Eventually, a gated community cannot keep the people outside the gates" Hatua hii inapofikiwa basi mwanzo wa mwisho wa jamii hiyo unakuwa umefikiwa. Mwandishi huyu anaamini kwamba dola kubwa la Maya lilianguka kwa sababu ya mapinduzi ya tabaka zalishi yaliyosababishwa na ubwete wa tabaka tawala ambalo kamwe halikuweza kushughulikia matatizo ya wananchi yakiwemo shida za kimazingira.

Niliondoka katika mhadhara huu nikiifikiria nchi yangu Tanzania na historia yake fupi. Je, tabaka la mabilionea wachache (wenye "vijisenti vyao") na tabaka la masikini wasio na kitu yatasimamiana na kukodoleana macho kwa amani mpaka lini? Je, utafika wakati ambapo tabaka zalishi litasema "sasa yatosha liwalo na liwe?" Nina matumaini kwamba hatutafikia hatua hii kwani ninaamini kwamba tunao viongozi makini ambao, kama kweli wanaitakia mema Tanzania a.k.a Kisiwa cha Amani, a.k.a Bongo, a.k.a. Nchi ya Vijisenti basi watahakikisha kwamba tabaka zalishi kamwe haligoti katika mwisho wa mwisho na kubwaga manyanga chini. Watahakikisha kwamba tabaka zalishi linaweza kupata elimu, afya pamoja na uhakika wa kujipatia mlo na mahitaji mengine ya lazima, hali ambayo italiwezesha kuendelea kuwa na matumaini ya kuishi na kuiona kesho. Kwa hali hiyo naamini na kutumaini kwamba Tanzania YENYE AMANI itaendelea kuwepo kesho na kesho kutwa. Mungu ibariki Tanzania!

Wednesday, April 15, 2009

RAISI WA BOLIVIA AMALIZA MGOMO WA KULA

Evo Molares - Rais wa Bolivia amemaliza mgomo wake wa kula uliodumu kwa siku sita. Raisi huyu machachari na mpigania haki za wazawa wa taifa lake alikuwa amegoma kula akilishurutisha Baraza la Kongresi la Bolivia kupitisha mabadiliko ya katiba ambayo, pamoja na mambo mengine, yatamruhusu kugombea tena uraisi kwa kipindi kingine cha miaka mitano. Raisi huyo alikuwa anapitisha muda wake akiwa amelala kwenye godoro lililokuwa limewekwa sebuleni katika makazi yake rasmi kama raisi wa Bolivia.

Katika siku hizo sita alikuwa anakunywa maji na kutafuna majani ya mmea wa Koka - ambao ndio malighafi-mama katika utengenezaji wa Cocaine. Mmea huo hutumiwa na wenyeji wengi wa Bolivia na nchi nyingine za Latin Amerika kama kizuia njaa ingawa Marekani inapigana vita vya kufa na kupona kujaribu kuuangamiza kabisa mmea huo.

Baada ya majadiliano makali hatimaye Baraza la Kongresi limepitisha mabadiliko hayo na sasa yuko huru kugombea tena uraisi. .

Nilikuwa sijawahi kusikia mgomo wa chakula ukitumiwa na kiongozi wa nchi kama silaha ya kubadilisha katiba ili kujiongezea muda wa kutawala. Sitashangaa mbinu hii ikiigwa na viongozi wa Afrika ingawa sina uhakika kama kweli wanaweza kukaa siku sita nzima bila kula.

Tuesday, April 14, 2009

Monday, April 13, 2009

TUTATUKUZA VYA WENGINE NA KUDHARAU VYA KWETU MPAKA LINI?

 
Makala haya yatatoka katika gazeti la Kwanza Jamii 
la Kesho Jumanne tarehe 14, 2009
 
Tutatukuza vya Wengine na Kudharau vya Kwetu Mpaka Lini?
Na Dkt. Masangu Matondo Nzuzullima  
  Marehemu Mariam Makeba katika wimbo wake mmoja analalamika kuhusu shujaa Shaka Zulu kuitwa Napoleoni Mweusi na Waingereza. Makeba anadai kwamba pengine Napoleoni alikuwa Shaka Zulu mweupe! Nimeshasikia pia Shaaban Robert – yule mwandishi bora kabisa katika fasihi ya Kiswahili – akilinganishwa na William Shakespeare, kingunge wa fasihi ya Kiingereza. Kwa mantiki hii nilianza pia kujiuliza: kwa nini William Shakespeare asiitwe Shaaban Robert mweupe?
Ulinganishaji wangu huu uliendelea kuimarishwa na kugunduliwa kwa mchoro asilia wa William Shakespeare mwezi jana kule Uingereza. Wapiga mnada walikuwa wanaamini kwamba kama mchoro huo ungepigwa mnada pengine ungeingiza mamilioni ya dola. Nilianza kujiuliza, mchoro asilia wa Shaaban Robert ukigunduliwa leo utauzwa kwa shilingi ngapi? Ni Watanzania wangapi wanafahamu Shaaban Robert alikuwa nani? Ni wangapi wanaoitambua sura yake wakiiona? Kuna anayejali?
Ninatumia mifano hii ya ulinganifu kuelezea jinsi utandawazi unavyoangamiza na kutokomeza tamaduni na historia zetu kwa kasi ya kutisha. Hili si jambo ambalo limetokea kwa kufumba na kufumbua. Hili ni tokeo la muda mrefu la mkakati maridadi wa watalawa wetu kuvuruga tamaduni zetu na hivyo kuharibu kujitambua kwetu na nafasi yetu katika dunia hii. Historia imeushuhudia utekelezaji wa mkakati huu huu katika hatua zake mbalimbali katika vipindi tofauti vya kihistoria.
Tunajua kwamba utumwa wetu wa fikra ulianzia katika matapo mbalimbali ya utandawazi yaliyotangulia, matapo ambayo yalitukutanisha na wageni kutoka Ulaya na kwingineko. Mahusiano yetu na ulimwengu wa wageni hawa kutoka nje daima yamekuwa ya kihasama, kiunyonyaji na dhuluma – kuanzia enzi za biashara ya utumwa mpaka wakati huu tulio nao. Uzalendo, utu na Uafrika wetu ulikunguwazwa na kufishwa wakati wa biashara ya utumwa “tulipokubali” kugeuzwa bidhaa na kuuzwa kama nyanya au vitunguu sokoni. Ni wakati huu ambapo tulipondwapondwa kisaikolojia na kuaminishwa kwamba tulikuwa binadamu wa tabaka la chini ambao kamwe tusingeweza kuwekwa katika daraja moja na “mabwana” kutoka Ulaya. Vita hivi vya kisaikolojia vilivyopiganwa kwa ujanja sana kupitia dini na sera za lugha dhidi yetu viliendelezwa na “mabwana” wakati wa ukoloni. Ni wakati huu ambapo bara letu liliitwa bara la giza na tamaduni zetu zilizotukuza, kutulea huku zikishabihiana vyema na mazingira yetu ya asili zilibatizwa kuwa za kishenzi na kinyama. Ukoloni ulitazamwa na hata kutambulishwa kama mkakati wa “kutustaarabisha” na kututoa katika giza nene la kuabudu dini za “kishenzi”, kuongea lugha za kishamba na kukumbatia tamaduni zetu za kiwango cha chini. Lugha zetu ambazo kupitia kwazo fikra zetu na mtazamo wetu pamoja na nafasi yetu katika dunia hii vimefinyangwa ziliitwa duni, zikadumazwa na kunyimwa nafasi za matumizi katika sekta rasmi. Matokeo yake lugha zetu ambazo ndizo zinaamua sisi ni nani na tunahusianaje na wengine katika mazingira yetu zilinyimwa “meno” na tangu hapo zimebakia kuwa lugha zisizo na mwelekeo wala matumaini. Kulingana na Ngugi wa Thiong’o, ukoloni na utumwa wetu wa kisaikolojia ulikamilika pale tulipokubali lugha zetu kuvishwa sanda na kutengwa na ulimwengu na mazingira yetu. Kuanzia hapo, tulikoma kuwa sisi na kuanzia wakati ule, sisi si sisi tena, hatujijui na hatujui kwamba hatujijui kuwa sisi ndisi. Tumekuwa watumwa wa fikra!
Kupatikana kwa uhuru (wa bendera) katika miaka ya sitini kulileta matumaini makubwa katika mioyo ya Waafrika. Iliaminika kwamba uhuru wa kisiasa ulikuwa ni hatua za mwanzo tu na ungefuatiwa na uhuru wa kiuchumi na kitamaduni. Ndiyo maana Kwame Nkrumah - raisi wa kwanza wa taifa huru la kwanza barani Afrika (Ghana) aliwatangazia Waafrika “kuutafuta kwanza uhuru wa kisiasa na uhuru mwingine ungefuata”. Baada ya miaka sitini ya uhuru, ni wazi kwamba tungali tunatawaliwa kiuchumi na uhuru uliotegemewa katika nyanja zingine za maisha yetu haujapatikana. Lakini utumwa mbaya kabisa ni ule utumwa wa kisaikolojia - utumwa wa kimawazo uliomdogosha Mwafrika na kumfanya ajione kuwa yeye ni binadamu wa daraja la pili na utamaduni wake kuwa wa kizamani, usioendana na wakati na wa kishenzi. Mkakati mama ulioanzishwa na watawala wetu wakati wa biashara ya utumwa na kuendelezwa (wakati mwingine kwa nguvu) wakati wa ukoloni bado unaimarika siku hadi siku na bado umejikita barabara katika fikra zetu. Na baada ya miaka sitini ya uhuru bado tunaamini kwamba lugha zetu ni za kishamba na hazifai kutumiwa katika sekta rasmi kama elimu na vyombo vya habari. Matokeo yake lugha zetu za jadi zimegeuka kuwa lugha za kuonewa haya na kizazi kipya hakitaki tena kuzizungumza. Sijui inamaanisha nini kuwa Msukuma wakati hujui Kisukuma na utamaduni wa Wasukuma. Ati, inamaanisha nini kuwa Mhehe wakati hujui Kihehe wala utamaduni wa Wahehe na mtazamo wao kuhusu maisha wala nafasi yao katika dunia hii? Je, Mfaransa anaweza kweli kudai kuwa yeye ni Mfaransa hata kama hajui lugha ya Kifaransa na utamaduni wa Wafaransa? Wanaisimu Sosholojia wengi wanaamini kwamba nyingi ya lugha zetu hizi ambazo sasa tunaziita eti za “kirugaruga” zitatokomea kati ya vizazi vitano hadi kumi vijavyo. Je, lugha zetu na utamaduni wetu utakapokufa, sisi tutakuwa nani katika dunia hii? Pengine sote tutakuwa “Waingereza!” 
Baada ya miaka sitini ya uhuru, bado hatuthamini akina Shaaban Robert wetu. Wakati Waingereza na Warusi wakiwatukuza na kuwaenzi akina William Shakespeare na Tolstoy wao, wakati Wachile wakimuenzi Pablo Neruda wao, sisi tunawaenzije akina Shaaban Robert wetu? Ati, tunawakumbuka na kuwaenzi akina Kinjeketile, Chifu Mkwawa na Mtemi Mirambo wetu kama akina David Livingstone na Karl Peters wanavyotukuzwa kule Ulaya? Tunao wasomi wazuri sana lakini kutokana na kutothaminiwa kwao wengi wao wanaishia kukimbilia nje ambako usomi na utaalamu wao unathaminiwa. Wasomi hawa wazawa hawalipwi mishahara kama wenzao kutoka Ulaya hata kama utaalamu wao unalingana, wamesoma katika vyuo vinavyolingana kwa hadhi na wanafanya kazi ile ile. Cha ajabu ni kwamba hakuna anayejali na inaonekana kama vile serikali zetu zinafurahia kuondoka kwao kwani kutokana na mwamko wao wa kisiasa hutazamwa na tabaka tawala kwa jicho la hati hati. Ni ndoto tu kufikiri kwamba tutaweza kuendelea bila kuwa na wataalamu wa kutosha katika nyanja zote muhimu kama vile elimu, afya, uhandisi n.k.
Ninapenda nimalizie makala hii na kisa hiki kilichonipata pale posta mpya jijini Dar es salaam. Nilikwenda pale kutafuta kadi mbalimbali za Valentine na Krismasi zilizoandikwa kwa Kiswahili kwa ajili ya kufundishia wanafunzi wageni. Cha ajabu ni kwamba kadi za Kiswahili zilikuwa hazipatikani. Niliambiwa kwamba kama nilikuwa nazihitaji ilikuwa lazima nifanye oda maalumu nikatengenezewe na hii ingechukua karibu wiki moja. Nilijaribu kuwauliza vijana mbalimbali ni kwa nini kadi za Kiswahili zilikuwa hazipatikani? Niliambiwa kwamba eti maneno “I Love you” hayatamkiki wala kusikika vizuri yakitamkwa kwa Kiswahili. Eti yanakosa “ladha” iliyokusudiwa na vijana wanapendelea kadi zilizoandikwa kwa Kiingereza hata kama hawafahamu Kiingereza. Lojiki hii kidogo ilinishangaza. Ninavyofahamu ni kwamba lugha zote hapa ulimwenguni zina msamiati wa kutosha kuelezea kila kitu kilichomo katika mazingira ya wazungumzaji wake. Lugha karibu zote zinayo namna ya kutamka “I love you”. Kwa mantiki hii hakuna sababu nyingine yenye mashiko inayoifanya “nakupenda” isiwe na “ladha” kama “I love you” mbali na utumwa wa fikra wa kudhani kwamba kwa vile Kiingereza ni lugha ya “mabwana” inayoshabihishwa na usasa na hadhi basi inaonekana kuwa bora kuliko lugha ya Kiswahili. Na kama Kiswahili kinaonekana duni na kukosa “ladha” mbele ya Kiingereza, je vipi kuhusu lugha zetu zingine zisizo na nguvu kama Kiswahili mf. Kisukuma, Kigogo na Kiha? 
Je, ni lini tutaendelea kutukuza vya wengine na kudharau vya kwetu? Ni kweli kwamba Ushaaban Robert wetu hauwezi kukamilika bila kulinganishwa na Shakespeare? Ni lazima Ushaka Zulu wetu ukamilishwe na Unapoleoni wao? Haya ni baadhi ya maswali ambayo inabidi tuanze kujiuliza tunapoanza kujitafuta na kujitambua upya sisi ni nani na nafasi yetu katika dunia hii ni ipi.
matondo.blogspot.com
profesamatondo@gmail.com

ELIMU YA JADI INAYOFIFIA

Kwa vile tumefundishwa kwamba ili kupata moto ni lazima uwe na kiberiti, wengi wetu tunaweza kufa na njaa kiberiti kikikosekana. Kwa vile tumefundishwa kwamba ili uweze kukoga ni lazima uende mtoni, kisimani au bafuni, wengi wetu tunaweza kufukuta kwa vile eti hakuna maji, lakini si kwa hawa Wasan wenyeji wa Jangwa la Kalahari. Elimu yao imewapa mbinu mbadala za kuweza kupambana na kuyamudu mazingira yao vizuri. Na hawa hawahitaji kukaa madarasani na kupata maPhD. Elimu yao ni hai na imefumana mumo kwa mumo na maisha na mazingira yao. Halafu mtu kutoka nje anakuja na kuiita elimu hii kuwa ya kishenzi! Ni aibu kubwa kwamba elimu hii ya jadi inazidi kuangamia na kufifia kwa kasi ya kutisha.

Wanaume hawahitaji kiberiti kukoka moto (Picha zote na Petri Kosina)


















Mizizi hii ina maji ya kutosha kunywa na hata kuoshea watoto!













Tuesday, April 7, 2009

HII NDIYO NJIA BORA KABISA YA KUFUNDISHIA HESABU

Kujumlisha, kutoa, kugawanya na hata kuzidisha vinaweza kufundishika kwa urahisi sana kwa njia hii - vyote katika mazingira yetu wenyewe. Kuna vingapi ambavyo tunaweza kuvifanya vikawa vyetu na tukafundishana kulingana na mazingira yetu, tukaepuka kukaririshana na kuumizana vichwa bure? Kuna ulazima kweli wa kukariri Hydrological Cycle? Mbona mtoto asiambiwe kuweka bakuli la maji katika jua halafu aone baada ya masaa manne kutatokea nini na aunde nadharia zake mweyewe kuelezea nini anafikiri kimetokea? Au akifumwa anadokoa mguu wa kuku jikoni, mbona asiulizwe kuelezea mvuke huo wa joto katika sufuria ulikotoka na unakoenda? Tuache kukaririshana bila sababu. Tukiweza kuwafanya watoto wetu wakaiona elimu kupitia jicho la mazingira yao wenyewe, utakuwa mwanzo wa mapinduzi makubwa sana katika elimu yetu. Hebu fikiria kama ungefundishwa Newton's Laws of Motion kwa njia hii!

Monday, April 6, 2009

MBUNGE WANGU NA MABILIONI YA WANANCHI

Lakini ukifika jimboni kwake hakuna lolote. Bilioni moja tu ingetosha kuchimba visima vya maji karibu katika vijiji vyote. Hii ingemfanya aingie katika Historia kwa kuwa mbunge wa kwanza kutumia pesa "zake" kuhakikisha kwamba jimbo lake lote lina maji safi. Kuna raha gani kukaa na mabilioni yote haya huku watu wako wakiwa hawana cho chote? Sitashangaa akishinda tena ubunge mwaka kesho na hata kuukwaa uwaziri tena! Katika uchaguzi uliopita alifanya kufuru kwa kugawa baisikeli, mabati, vitenge, sukari, chumvi, pesa, kanga na hata pikipiki. Bado changamoto tuliyonayo ni kubwa!

WACHAGA HAPA MNASEMAJE?






Scan ya gazeti kutoka kwa Kennedy

Wednesday, April 1, 2009

CHANGAMOTO YETU...

Baba kakaa na kupiga akili akaona hakuna "option" na akaamua kumtia mtoto wake kwenye tenga ambalo kwa kawaida hutumika kusafirishia wanyama kama mbuzi na kondoo tena ambao mara nyingi wanakwenda kuchinjwa. Sikuweza kuipata habari hii kamili lakini natumaini huyu mtoto alipona na siku moja atakuja kusimulia kisa hiki. Hii ni changamoto yetu sote kwani sidhani kama ni sahihi katika karne hii ya 21 tuendelee kusafirisha wagonjwa wetu katika matenga!

ELIMU YA JADI, FALSAFA YA ASILI NA "USASA"

Wazungu walifanikiwa kutuaminisha kwamba kabla ya kufika kwao hatukuwa na elimu. Wakatuchezea fikra zetu na kutufanya tuamini kabisa kwamba walikuwa wametuletea "mwanga" Baada ya kuisoma hadithi hii ya Marafiki Watatu na Simba ambayo inapatikana katika kitabu hiki, mara moja utagundua kwamba hata kabla ya mawasiliano yetu na 'wagawa ustaarabu" kutoka Ulaya tulikuwa na elimu iliyokomaa, ya kweli na iliyoshabihiana na mazingira yetu. Nimeikumbuka hadithi hii baada ya kuona mijadala ambayo imekuwa ikirindima katika blogu mbalimbali katika kujaribu kuelezea "msomi ni nani?" na athari za wasomi katika jamii. Na kwa mara ya kwanza inabidi nikubaliane na Kamala ambaye haamini "kabisa kwamba ili uwe msomi unahitaji vyeti na kuvuka madaraja..." Isome hadithi hii fupi hapa chini
======================================

Marafiki Watatu na Simba

Hapo kale palikuwa na watu marafiki watatu. Marafiki hawa walisoma sana na wali­kuwa na maarifa sana ya namna mbalimbali, lakini hawakuwa na hekima. Watu hawa watatu walikuwa na rafiki yao mmoja. Rafiki huyu hakusoma sana lakini alikuwa na hekima nyingi.


Wakati mmoja, mmoja wao aliwaambia wenzake wasafiri ili waonyeshe uhodari wao. Wote wakakubali lakini wawili walikataa kumchukua rafiki yao wa nne kwa sababu hakuwa na maarifa. Rafiki wa tatu akasema afadhali wamchukue. Basi wale wawili wakakubali.


Wakaenda mpaka porini. Hapo wakaona ngozi na mifupa ya simba mfu. Mmoja mio­ngoni mwa wale marafiki wenye maarifa akasema sasa wataonyesha uhodari wao kwa kumtia uhai yule simba. Akasema yeye ataweka mifupa yake pamoja. Wa pili akasema atamtia nyama, damu na ngozi nzuri, na wa tatu atamrudishia uzima wake. Mtu wa nne mwenye hekima na bila maarifa akasema kwamba simba atakuja kuwaua. Lakini hawa­kumsikiliza. Basi yeye akapanda juu ya mti.


Wale watatu wakamtia simba uhai. Yule simba akawa hai na tena mkali sana. Aka­warukia na kuwaua wale watatu mara moja. Ukawa ndio mwisho wa maarifa yao. Yule mwenzao alikaa kimya mpaka simba akaenda zake. Akashuka mtini na kurudi kwao.

JIANDIKISHE HAPA

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

BLOGU ZA BURUDANI NA UREMBO