- Japo leo ni siku ya wanaume duniani, kuko kimyaaaaa na sijasikia cho chote kwenye redio na vyombo vingine vya habari kuhusu siku hii muhimu. Naamini ingekuwa siku ya wanawake basi tungesikia "makelele" ya kila aina kutoka kila kona.
- Mbona siku yetu akina baba inadharauliwa namna hii? Au kwa vile ni sikukuu iliyoanza hivi karibuni tu (2009)? Au ni kwa vile hatuna mchango muhimu katika jamii mbali na kuanzisha migogoro na vita, kuendeleza mifumo dume yenye kunyanyasa akina mama na masaibu mengineyo?
- Nimefurahi kusikia kwamba sikukuu hii imesherehekewa Tanzania kwa kuanzisha rasmi Chama Cha Wanaume Wanaopigwa Tanzania (CCWWT). Baadhi ya kanuni za chama hiki zinapatikana hapa (ucheshi).
- Hongereni wanaume popote mlipo hapa duniani; na hasa akina baba mnaoshiriki kikamilifu katika malezi ya watoto kama huyo juu katika kibonzo.





Hawa wanaume wanaodundwa na wake zao katika ndoa wanatuaibisha. Niko tayari kuwafundisha karate na makandokando bure! Watu wazima hovyo!!!
ReplyDeleteWe anony. hapo juu you don't know what you are saying. Kuna mijimama inajua ngumi na vichwa ka vile midume. Ukikumbana nayo hata wewe mwenye kareti na hayo sijui makandokando yako utachemsha tu.
ReplyDeleteMwanaume unadundwa halafu ukitaka uende polisi unakatiwa mauno, even tigo unapata, majeraha yanakandwa maji na kukandikwa mabandeji kibao maneno kwisha. Next time ukichemsha unadundwa tena - and the cycle goes on and on. Afadhali tuwe na chama chetu kitusaidie...I like the idea.
Hao wanaume si wanaume kiukweli wana matatizo ,mwanamke haswa hawezi kumpiga mwanamme ,mwanamke mwenyewe basi mmmmhhh
ReplyDeletekaka nimeiona sasa! asante sana.Je hiki chama kinaendelea?
ReplyDelete