- Vuguvugu la kudai katiba mpya limepamba moto nchini Tanzania. Sijui ni wangapi wanaoshiriki katika vuguvugu hili wameshawahi kuisoma katiba nzima na kutafakari mapungufu yake. Hapa chini ni katiba nzima kama ilivyowekwa katika tovuti ya Wizara ya Mambo ya Katiba. Hebu na tuisome kwa makini kabla hatujaamua ni mabadiliko gani tunayotaka kuyafanya. Mungu Ibariki Tanzania!!!
Au unaweza pia kutembelea hapa... (Kutoka udadisi)
TOLEO LA MWAKA 2000 LA KATIBA:
http://groups.yahoo.com/group/Wanazuoni/message/8085
MABADILIKO YA TOLEO LA MWAKA 2005 LA KATIBA:http://groups.yahoo.com/group/Wanazuoni/message/8138
MABADILIKO YA TOLEO LA MWAKA 2005 LA KATIBA:http://groups.yahoo.com/group/Wanazuoni/message/8138





Tatizo ni kwamba hata KATIBA ya zamani waliowengi hawaifahamu. Kwa mawazo yangu badala ya kutaka ibadilishwe ni bora kwanza ingewekwa wazi na kufafanuliwa kwa watu wote ili kwamba kama kuna upungufu marekebisho au kuwa na mpya kabisa iwe hivyo kulikoni wanasiasa wachache walioona hizo kasoro na kutaka wkubadilisha.
ReplyDeleteNi vyema tukatumia mwaka mzima wa 2011 kuelezana kuhusu katiba iliyopo ili katika muda huo tuone ni kipi cha kuondoa au kuongeza.
Nikweli mwana!
ReplyDeleteMimi hiyo nimeiona kuna watu wengi hiyo Katiba yenyewe hatuijui kama vipi mpango mzima kwanza tuijue wote ndipo tuibadilishe.
Sasa wakija kunihoji sina jibu kipi kibadilishwe.