- Mbali na nyimbo kombozi na za kiharakati za "Reggae", mimi hupenda sana nyimbo za "Country" kwani zimejaa hadithi za kweli, visa, misukosuko, shangwe, ushindi na hata huzuni na maanguko yetu hapa duniani kama binadamu.
- Ijumaa ya leo na wikiendi hii kwa ujumla napenda kuwashirikisha katika wimbo huu niupendao sana wa "God Blessed the Broken Road", wimbo ulioimbwa na bendi mashuhuri ya Rascal Flatts. Huwa napenda kuusikiliza wimbo huu nikiwa faraghani, na japo ni wimbo wa mapenzi, daima hunijaza fikra mpya, kunifurahisha na hata kuniliza na hatimaye kunipatia "utakaso (catharsis)" ambao hunifanya niyatazame maisha upya na safari yangu hapa duniani kwani wakati mwingine binadamu sie inatubidi tupite katika barabara zilizopondeka ili kufika tunakojaribu kwenda.
- Maisha yetu ni kama muziki. Na kila siku mstari mmoja mmoja unanyofolewa, na kabla hatujakaa sawa tunashtukia ubeti mzima umekwisha. Leo tunamaliza ubeti mmoja na kesho tunaanza ubeti mwingine katika nyimbo zetu za maisha. Tatizo ni kwamba hatukupewa uwezo wa kufahamu idadi ya mistari na beti zilizobakia kabla ya nyimbo zetu kufikia kikomo. Kwa hivyo tunakwenda tu kwa kubahatisha huku tukipapasapapasa huku na huko tukwa tumefungwa macho.
- Hebu Mungu na Akaibariki barabara yako iliyopondeka unayoipitia kwa wakati huu. Kaza macho upeoni na kamwe usitawe na kuiacha safari kwani inawezekana ili kufika huko uendako, ni lazima uipitie barabara hii kwa wakati huu. Safari ni lazima iendelee ati! Tunakutakia wikiendi njema sana. Upendo na ukatawale daima !!!
**************
Mashairi ya Wimbo huu
"Bless The Broken Road"
I set out on a narrow way many years ago
Hoping I would find true love along the broken road
But I got lost a time or two
Wiped my brow and kept pushing through
I couldn't see how every sign pointed straight to you
I set out on a narrow way many years ago
Hoping I would find true love along the broken road
But I got lost a time or two
Wiped my brow and kept pushing through
I couldn't see how every sign pointed straight to you
[Chorus:]
Every long lost dream led me to where you are
Others who broke my heart they were like Northern stars
Pointing me on my way into your loving arms
This much I know is true
That God blessed the broken road
That led me straight to you
I think about the years I spent just passing through
I'd like to have the time I lost and give it back to you
But you just smile and take my hand
You've been there you understand
It's all part of a grander plan that is coming true
[Chorus]
I'd like to have the time I lost and give it back to you
But you just smile and take my hand
You've been there you understand
It's all part of a grander plan that is coming true
[Chorus]
Now I'm just rolling home
Into my lover's arms
This much I know is true
That God blessed the broken road
That led me straight to you
That God blessed the broken road
That led me straight to you.
Into my lover's arms
This much I know is true
That God blessed the broken road
That led me straight to you
That God blessed the broken road
That led me straight to you.
**************
Mashairi katika Kiswahili
"Mungu Ibariki Barabara Iliyopondeka"
(Tafsiri yangu ya haraka haraka)
Na Rascal Flatts
Ubeti wa Kwanza
Miaka mingi iliyopita
Niliazimia kuifuata njia nyembamba
Nikitumaini kukutana na mapenzi ya kweli
Katika barabara iliyopondeka
Ingawa niliishia kupotea hapa na pale
Nilijifuta kope zangu
Na kuendelea na safari yangu
Japo sikuweza kuona kwamba
Kila ishara, ilinielekeza kwako moja kwa moja
(Tafsiri yangu ya haraka haraka)
Na Rascal Flatts
Ubeti wa Kwanza
Miaka mingi iliyopita
Niliazimia kuifuata njia nyembamba
Nikitumaini kukutana na mapenzi ya kweli
Katika barabara iliyopondeka
Ingawa niliishia kupotea hapa na pale
Nilijifuta kope zangu
Na kuendelea na safari yangu
Japo sikuweza kuona kwamba
Kila ishara, ilinielekeza kwako moja kwa moja
Korasi
Kila ndoto ndefu iliyopotea
Iliniongoza kuja kwako
Na wengine walioumiza moyo wangu
Walionekana kama nyota za Kaskazini
Zilizonionyesha njia
Ielekeayo katika mikono yako ya upendo
Na hiki ndicho nikijuacho kwamba ni kweli
Kwamba Mungu Aliibariki ile barabara iliyopondeka
Iliyoniongoza moja kwa moja
Kuja mikononi mwako
Kila ndoto ndefu iliyopotea
Iliniongoza kuja kwako
Na wengine walioumiza moyo wangu
Walionekana kama nyota za Kaskazini
Zilizonionyesha njia
Ielekeayo katika mikono yako ya upendo
Na hiki ndicho nikijuacho kwamba ni kweli
Kwamba Mungu Aliibariki ile barabara iliyopondeka
Iliyoniongoza moja kwa moja
Kuja mikononi mwako
Ubeti wa Pili
Ninawaza miaka niliyopoteza nikizururazurura
Na ningependa kuufidia muda nilioupoteza wakati huo
Kwa kuwa pamoja nawe
Lakini wewe huishia kutabasamu tu
Na kuushika mkono wangu
Kwani umeshayapitia hayo
Na unaelewa kwamba
Yote haya ni sehemu ya Mpango Mkuu
Ambao sasa unatimia
Korasi
Na sasa niko naseserea kuja nyumbani
Kwenye fumbato la mpendwa wangu
Na hiki ndicho nikijuacho kuwa ni kweli:
Kwamba Mungu Aliibariki ile barabara iliyopondeka
Iliyoniongoza moja kwa moja
Kuja mikononi mwako
Ninawaza miaka niliyopoteza nikizururazurura
Na ningependa kuufidia muda nilioupoteza wakati huo
Kwa kuwa pamoja nawe
Lakini wewe huishia kutabasamu tu
Na kuushika mkono wangu
Kwani umeshayapitia hayo
Na unaelewa kwamba
Yote haya ni sehemu ya Mpango Mkuu
Ambao sasa unatimia
Korasi
Na sasa niko naseserea kuja nyumbani
Kwenye fumbato la mpendwa wangu
Na hiki ndicho nikijuacho kuwa ni kweli:
Kwamba Mungu Aliibariki ile barabara iliyopondeka
Iliyoniongoza moja kwa moja
Kuja mikononi mwako
**************
Wimbo na Mashairi pamoja




Mmmh!
ReplyDeleteOooohhhh! mai gash! Matondo umenikuna penyewe. UPENDO UDUMU MILELE, PANAPOKOSEKA UPENDO YOTE HUHARIBIKA. HATA YULE MWENZA ULKIYEMPENDA KUPITA VYOTE HUMUONA NI SUMU.
ReplyDeleteUBARIKIWE KWA WIMBO HUU PAMOJA TA TAFSIRI YAKE