- Pamoja na changamoto zote zinazokikabili, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimetamba barani Afrika kwa kushika nafasi ya 36 kwa ubora katika ripoti iliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la URAP. Kiulimwengu kimeshika nafasi ya 1593.
- Vyuo vikuu vingine vya Tanzania vilivyotajwa katika ripoti hiyo ni Muhimbili (42 barani Afrika, 1,716 kiulimwengu) na Sokoinne (45 barani Afrika, 1,771 kiulimwengu). Chuo Kikuu cha Capetown nchini Afrika Kusini ndicho kimeshika nafasi ya kwanza barani Afrika na kama kawaida Chuo Kikuu cha Harvard nchini Marekani kimeshika nafasi ya kwanza kiulimwengu.



Wow hongera sana chuo kikuuu... What a milestone for our Uni!!! Thank you for this article....
ReplyDelete